John 6:1-6

Isa Alisha Wanaume 5,000

(Mathayo 14:13-21; Marko 6:30-44; Luka 9:10-17)

1 aBaada ya haya, Isa alikwenda ng’ambo ya Bahari ya Galilaya, ambayo pia huitwa Bahari ya Tiberia. 2 bUmati mkubwa wa watu uliendelea kumfuata, kwa sababu waliona ishara nyingi za miujiza alizofanya kwa wagonjwa. 3 cKisha Isa akapanda mlimani akaketi huko pamoja na wanafunzi wake. 4 dPasaka ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.

5 eIsa alipotazama na kuuona ule umati mkubwa wa watu ukimjia, akamwambia Filipo, “Tutanunua wapi mikate ili watu hawa wale?” 6Aliuliza swali hili kumpima, kwa maana alishajua la kufanya.

Copyright information for SwhKC